Baraza
Baraza la Manispaa Kati
Zanzibar
SMZ
Baraza la Manispaa Kati
+255 773 168 121
|

Madiwani ni wawakilishi wa wananchi waliochaguliwa katika majimbo mbalimbali ya Wilaya ya Kati. Wanafanya kazi ya kutunga sheria na kusimamia utekelezaji wa mipango ya maendeleo.

16
Madiwani Wote
10
Majimbo
Sheria Na. 17 ya Mwaka 2014

Muundo wa Baraza la Madiwani

Kwa mujibu wa Sheria Na. 17 ya mwaka 2014, Baraza la Manispaa Kati lina aina tatu za madiwani:

Madiwani wa Kuchaguliwa

Madiwani wanaochaguliwa na wananchi kutoka katika wadi 8 za Wilaya ya Kati:

Cheju Koani Bambi Tunguu Ubago Chwaka Bungi Kiboje

Madiwani Wateule

Madiwani 5 wanaoteuliwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Vikosi Maalum vya SMZ.

Viti Maalum vya Wanawake

Madiwani watatu (3) wa viti maalum vya wanawake.

Meya wa Baraza la Manispaa Kati

Mhe. Said Hassan Shaaban

Jimbo la Wadi ya Koani

Mhe. Said Hassan Shaaban ni Diwani wa Wadi ya Koani katika Wilaya ya Kati, Unguja. Pia anahudumu kama Meya wa Baraza la Manispaa Kati. Katika nafsi yake ya uongozi, anawajibika kuwakilisha wananchi wa Wadi ya Koani, kushauri na kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo, na kushiriki maamuzi yanayohusu maendeleo ya Manispaa na Wilaya ya Kati.

Diwani wa Wadi ya Kiboje

Mhe. Haji Mzee Ali

Jimbo la Wadi ya Kiboje

Mhe. Haji Mzee Ali ni Diwani wa Wadi ya Kiboje. Ni kiongozi aliyechaguliwa na wananchi wa Wadi ya Kiboje kuwakilisha maslahi yao katika Baraza la Manispaa Kati na kusimamia utekelezaji wa shughuli za maendeleo katika wadi hiyo.

Diwani wa Wadi ya Bambi

Mhe. Abdulrahman Ali Abdalla

Jimbo la Wadi ya Bambi

Mhe. Abdulrahman Ali Abdalla, Diwani wa Wadi ya Bambi, ni mwakilishi wa wakazi wa Bambi aliyechaguliwa kusimamia na kulinda maslahi ya wakazi wa wadi hiyo katika Baraza la Manispaa Kati. Anawajibika kuratibu na kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kuhimiza ushiriki wa wananchi wa Bambi katika shughuli za kijamii na kiuchumi, pamoja na kushughulikia changamoto zinazowakabili wakazi wa wadi hiyo.

Diwani wa Wadi ya Bungi

Mhe. Seif Hamad Seif

Jimbo la Wadi ya Bungi

Mhe. Seif Hamad Seif ni Diwani aliyechaguliwa na wananchi wa Wadi ya Bungi. Anashiriki kikamilifu katika vikao vya Baraza la Madiwani na anachangia mipango ya maendeleo, ushauri na usimamizi wa shughuli za Manispaa kwa manufaa ya wananchi wa wadi yake.

Diwani wa Wadi ya Cheju

Mhe. Hamida Bahati Giri

Jimbo la Wadi ya Cheju

Mhe. Hamida Bahati Giri ni Diwani wa Wadi ya Cheju. Anajitahidi kuwakilisha maslahi ya wananchi wa Wadi ya Cheju katika Baraza la Manispaa Kati na kushiriki katika kupanga na kusimamia miradi ya maendeleo.

Diwani wa Wadi ya Chwaka

Mhe. Ali Hassan Mambo

Jimbo la Wadi ya Chwaka

Mhe. Ali Hassan Mambo ni Diwani wa Wadi ya Chwaka. Anawakilisha maslahi ya wananchi wa Wadi ya Chwaka na kushiriki kikamilifu katika maamuzi ya Baraza la Manispaa Kati yanayohusu maendeleo ya wilaya.

Naibu Meya wa Baraza la Manispaa Kati

Mhe. Hadhar Abdalla Hadhar

Jimbo la Wadi ya Tunguu

Mhe. Hadhar Abdalla Hadhar ni Diwani wa Wadi ya Tunguu na pia anahudumu kama Naibu Meya wa Baraza la Manispaa Kati. Anashiriki katika uongozi wa Baraza na kusimamia maendeleo ya Wadi ya Tunguu na Wilaya ya Kati kwa ujumla.

Diwani wa Wadi ya Ubago

Mhe. Ussi Mtumwa Ali

Jimbo la Wadi ya Ubago

Mhe. Ussi Mtumwa Ali ni Diwani wa Wadi ya Ubago. Anawakilisha wananchi wa Wadi ya Ubago na kushiriki katika mipango na maamuzi ya Baraza la Manispaa Kati.

Diwani wa Kiti Maalum

Mhe. Hidaya Said Hamad

Jimbo la Kiti Maalum

Diwani wa Kiti Maalum anashiriki kikamilifu katika vikao vya Baraza la Madiwani na anachangia mipango, ushauri na usimamizi wa utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa manufaa ya wananchi.

Diwani wa Kiti Maalum

Mhe. Tendani Mkanga Miraji

Jimbo la Kiti Maalum

Diwani wa Kiti Maalum anashiriki kikamilifu katika vikao vya Baraza la Madiwani na anachangia mipango, ushauri na usimamizi wa utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa manufaa ya wananchi.

Diwani wa Kiti Maalum

Mhe. Riziki Abdalla Mohamed

Jimbo la Kiti Maalum

Diwani wa Kiti Maalum anashiriki kikamilifu katika vikao vya Baraza la Madiwani na anachangia mipango, ushauri na usimamizi wa utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa manufaa ya wananchi.

Diwani wa Uteuzi wa Waziri

Mhe. Said Mtaji Askari

Jimbo la Uteuzi wa Waziri

Diwani wa Uteuzi wa Waziri ni mwanachama wa Baraza la Madiwani aliyeteuliwa na Waziri anayehusika na Serikali za Mitaa kwa mujibu wa sheria husika. Uteuzi huu unafanywa kwa lengo la kuimarisha uwakilishi, kuongeza utaalamu katika masuala ya maendeleo, na kuchangia uongozi na usimamizi wa shughuli za baraza au manispaa.

Diwani wa Uteuzi wa Waziri

Mhe. Catherine Peter Nao

Jimbo la Uteuzi wa Waziri

Diwani wa Uteuzi wa Waziri ni mwanachama wa Baraza la Madiwani aliyeteuliwa na Waziri anayehusika na Serikali za Mitaa kwa mujibu wa sheria husika. Uteuzi huu unafanywa kwa lengo la kuimarisha uwakilishi, kuongeza utaalamu katika masuala ya maendeleo, na kuchangia uongozi na usimamizi wa shughuli za baraza au manispaa.

Diwani wa Uteuzi wa Waziri

Mhe. Amina Adrew Clement

Jimbo la Uteuzi wa Waziri

Diwani wa Uteuzi wa Waziri ni mwanachama wa Baraza la Madiwani aliyeteuliwa na Waziri anayehusika na Serikali za Mitaa kwa mujibu wa sheria husika. Uteuzi huu unafanywa kwa lengo la kuimarisha uwakilishi, kuongeza utaalamu katika masuala ya maendeleo, na kuchangia uongozi na usimamizi wa shughuli za baraza au manispaa.

Diwani wa Uteuzi wa Waziri

Mhe. Ghania Ali Makame

Jimbo la Uteuzi wa Waziri

Diwani wa Uteuzi wa Waziri ni mwanachama wa Baraza la Madiwani aliyeteuliwa na Waziri anayehusika na Serikali za Mitaa kwa mujibu wa sheria husika. Uteuzi huu unafanywa kwa lengo la kuimarisha uwakilishi, kuongeza utaalamu katika masuala ya maendeleo, na kuchangia uongozi na usimamizi wa shughuli za baraza au manispaa.

Diwani wa Uteuzi wa Waziri

Mhe. Juma Kumba

Jimbo la Uteuzi wa Waziri

Diwani wa Uteuzi wa Waziri ni mwanachama wa Baraza la Madiwani aliyeteuliwa na Waziri anayehusika na Serikali za Mitaa kwa mujibu wa sheria husika. Uteuzi huu unafanywa kwa lengo la kuimarisha uwakilishi, kuongeza utaalamu katika masuala ya maendeleo, na kuchangia uongozi na usimamizi wa shughuli za baraza au manispaa.